Bunda FM Radio

Mama ahukumiwa miezi sita nje ya jela wilayani Bunda kwa ukatili

April 30, 2025, 1:34 pm

Mahakama ya Wilaya ya Bunda ambapo hukumu imetolewa. Picha na Amos Marwa

 ‘‘Naomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwefundisho kwa jamii kuacha tabia ya ukatili dhidi ya  watoto’’. Aristariko Msongelo mwendesha mashitaka wa Jamhuri Wilaya ya Bunda.

Na Adolf Mwolo

Mahakama wilayani Bunda imemhukumu kifungo cha miezi 6 cha nje ya jela Neema Msimu John(28),Mkazi wa mtaa wa Mapinduzi kwa kosa la ukatali dhidi ya mtoto wake mwenye umri wa miaka minne kwa kumchoma moto kwenye mkono wake wa kushoto kwa kosa la kujisaidia hovyo.

Hukumu hiyo imetolewa Aprili 29, 2025  na Hakimu Mwandamizi,Betron Sokanya, baada ya mshitakiwa kukiri kutenda kosa hilo ambalo ni kinyume na kifungu C169A(1)  na (2) cha kanuni ya adhabu ya sura ya 16 iliyofanyiwa marejeleo mwaka 2022.

Frolence Debogo Afisa ustawi wa jamii Wilaya ya Bunda akizungumza na Bunda FM Radio nje ya mahakama baada ya hukumu kutolewa. Picha na Amos Marwa.

Awali kabla ya hukumu kutolewa, mwendesha Mashtaka wa Jamuhuri Aristariko Msongelo ameiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa ili iwefundisho kwa jamii kuacha tabia ya ukatili dhidi ya watoto.

Aidha Afisa ustawi wa jamii Wilaya ya Bunda Florence Debogo awewaasa wazazi kutotumia adhabu kali kwa watoto na badala yake watumie adhabu mbadala kama kumnyima mtoto kuangalia television na kuto kwenda kucheza ili kupunguza wimbi la ukatili kwa watoto.

Sauti ya Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Bunda Frolence Debogo

Kwa upande mwingine baadhi ya wazazi na wananchi wilayani Bunda wamewashauri wazazi wenzao na jamii kwa ujumla kuacha kutoa adhabu kali kwa watoto ambazo zinapindukia na kuwa ukatili

Sauti za baadhi ya wananchi waliotoa maoni yao kuhusu adhabu kwa watoto

Baadhi ya wazazi waliotoa maoni yao kuhusu malezi na hukumu ya ukatili dhidi ya watoto iliyotolewa na mahakama ya Wilaya Bunda. Picha na Amos Marwa