Uyui FM Radio

Wananchi ManiSpaa ya Tabora waendelea kumuenzi Hayati Dkt JOHN MAGUFULI

24 March 2021, 1:14 pm

Jamii katika Manispaa ya Tabora imesema inamuenzi na  itaendelea kumkumbuka aliyekuwa Raisi wa awamu ya tano  katika Jamuhuri ya muungano wa Tanzania  hayati Dkt John Pombe Magufuli  kwa juhudi na uchapakazi wake  ikiwa ni pamoja na  kuhakikisha watanzania wanapata huduma bora za kijamii.

mmoja wa wananchi akisaini kitabu cha maombolezo

 Hayo yamebainishwa na baadhi ya wakaazi wa  Manipsaa ya Tabora waliofika na kusaini kitabu cha maombolezo  cha hayati Dkt John Magufuli  katika Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tabora .

Christopha David,Husein Katanga  na Gorge Nsunzu  ambao ni baadhi ya wananchi hao wamesema  hayati Dkt Magufuli alikuwa  mchapakazi aliyelenga matokeo chanya  katika utendaji kazi wake.

Insert…wananchi….dak…1

sauti za wananchi

Akizungumzia  namna  ambavyo Hayati Dkt john  Mahufuli alivyo watumikia wanachi  enzi za uhai wake,Mratibu wa huduma ya afya ya uzazi mkoa wa Tabora Marselina Mpandachalo amesema huduma za afya zimeboreshwa huku akiahidi kushirikiana na Rais mpya  wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania mheshimiwa Samia Suluhu Hassani.

Insert…..mpandachalo……dak…2

sauti ya mratibu wa huduma za afya na uzazi Mkoa wa Tabora