Uvinza Fm

Waziri mkuu amewahakikishia wakulima wa mazao ya kimkakati masoko

16/09/2021, 9:10 pm

Na,Glory Paschal

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Mjaliwa Kassim amewahakikishia wakulima wanaolima mazao ya kimakakati nchini kuwawezesha katika mchakato wa kuandaa kulima na kuwatafutia masoko ya ndani na nje ya nchi.

Ametoa kauli hiyo alipotembelea Shamba la michikichi katika  kambi ya JKT Burombola iliyopo wilayani Kigoma na kusisitiza kuwa mazao yote tisa ya kimakakati nchini yapo chini ya uangalizi wa serikali kuhakikisha yanaleta tija kwa uchumi wa nchi na mkulima mmoja mmoja.

Amesema serikali imeamua kuongeza Mazao ya kimakakati kufikia tisa lengo ni kuongeza tija katika mazao ya kibiashara yatakayoiwezesha nchi kimapato na kutimiza hilo wakulima watasimamiwa katika maeneo yao ili kuhakikisha uzalishaji wake unakidhi mahitaji ya soko.

Sauti ya waziri mkuu wa Tanzania

Mkuu wa  Kambi ya JKT Burombola Iliyopo Wilayani Kigoma mkoani hapa amesema tayari hekari 500 zimeshaandaliwa na kupandwa lengo likiwa ni kufikia hekali 2000.

Sauti ya mkuu wa kambi ya JKT Burombola