Kuwahi mapema kliniki kwa mama mjamzito husaidia kiafya
09/09/2021, 5:54 pm
Na,Editha Edward
Imeelezwa kuwa kuwahi mapema kliniki kwa mama mjamzito humsaidia kujua hali ya mama kiafya Pamoja na hali ya mtoto wake aliyeko tumboni
Akizungumza na redio Uvinza fm mganga mkuu wilaya ya Uvinza dkt ZAITUNI HAMZA amesema kuna baadhi ya akina mama ambao hupuuzia kwenda kliniki pale wanapojitambua ni wajawazito kitendo ambacho hakikubaliki kiafya
Dkt ZAITUN ameongeza kuwa kwa sasa serikali imeweka mkakati wa kumfatilia kila mama mmoja mmoja kwenye kila Kijiji ili kubainisha mama ambaye ana ujauzito na hajafika kliniki ili aanze kwenda lengo likiwa ni kumvusha salama mama mjamzito hadi pale atakapojifungua
Baadhi ya akina mama wilayani hapa wameeleza faida za kwenda kliniki mapema
Hata hivyo Shirika la afya duniani WHO linashauri mama kwenda kliniki kuanzia mara nne katika kipindi chote cha ujauzito ili kufanyiwa vipimo na matibabu ya afya ya mama na mtoto kwa ujumla.