Uvinza Fm

Uharibifu wa miundombinu ya maji mkongoro bado unaendelea

07/09/2021, 8:17 pm

Na,Glory Paschal

Licha ya Kuundwa Jumuiya za watumia maji katika baadhi ya kata Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma  kwa lengo la kutoa taarifa ya uharibifu wa miundombinu ya maji katika mradi wa Maji wa Mkongoro Namba mbili bado uharibifu unaendelea.

Hayo yambainishwa na Meneja wa wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA, Mhandisi RESPISIUS MWOMBEKI , ambapo amesema baadhi ya watu wasio waminifu wamekuwa wakiharibu Miundombinu hiyo hali inayorudisha nyuma maendeleo.

sauti ya meneja wa maji safi na usafi wa mazingira

Mwenyekiti wa Jumuiya  hiyo Bw. BONIPHAS CHUZURA , ameyataja Maeneo ambayo bado   yanaongoza kwa uharibifu huo Ikiwemo Kata ya Simbo hali inayosababisha ukosefu wa maji kuendelea kuwepo.

Sauti ya mwenyekiti wa jumuiya

Naye Mratibu  wa Mradi wa Maji wa  Mkongoro namba mbili Bw. ABEL LUTEMBA mesema ili kuondoa hali hiyo kuna kila sababu ya kuweka ulinzi shirikishi itakayojumuisha kundi la  Jumuiya hizo za watumia maji na wananchi.