Uvinza Fm

Wazazi na walezi washauriwa kutowaruhusu watoto kusafirishwa

19/08/2021, 4:23 pm

Na,Glory Paschal

Wazazi na Walezi Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma wameshauriwa kutoruhusu watoto wao kusafirishwa kwenda kutumikishwa katika shughuli mbalimbali kinyume cha sheria

Afisa Ustawi wa Jamii halmashauri ya wilaya Kakonko  Bw. Mohamed Shauri  amesema baadhi ya wazazi na walezi wamekuwa wakishawishika na kuwaruhusu watoto wao kwenda kutumikishwa katika  shughuli mbalimbali za kiuchumi

Sauti ya afisa ustawi wa jamii kakonko

Hata hivyo redio uvinza imefanikiwa kuzungumza na mzazi ambaye aliruhusu mwanae wa kike mwenye umri wa miaka 14 kwenda kutumikishwa  katika kazi  za  ndani Huko Jijini Dar es Salaam ambapo amesema ni mwaka wa tatu sasa hana mawasiliano na mwanaye wala hajui mtoto huyo anaishije

Sauti ya mzazi

Nao baadhi ya wananchi wa wilaya za kakonko na kibondo wameitaka Serikali kuwachukulia hatua za kisheria madalali wanaobainika kuwasafirisha watoto hao

sauti za wananchi

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Kakonko, Kanali Evance Mesha Masala amesema idadi ya watoto wanaosafirishwa kwenda Mwanza ni kubwa licha ya kuwa ni kinyume cha sheria na kwamba  viongozi na jamii wanapaswa  kudhibiti vitendo hivyo.

sauti ya mkuu wa wilaya ya kakonko