Uvinza Fm

Wananchi walia na ukosefu wa maji

12/08/2021, 4:31 pm

Na,Mwanaid Suleiman

Wakazi wa kijiji cha Ruchugi Wilayani Uvinza mkoani Kigoma wameiomba serikali kutataua changamoto ya maji inayowakumba katika kijiji hicho  hasa katika kipindi cha kiangazi

Hayo yamesemwa na baadhi ya wakazi wa kijiji cha Ruchugi kuwa changamoto hiyo imekua kero  kwa muda mrefu huku wakihitaji serikali iwasaidie kusambaza mabomba kwa wingi na kuepusha kufuata maji kwa umbali mrefu

Sauti za wananchi

Akizungumza na redio Uvinza fm mwenyekiti wa kijiji cha Ruchugi  bw Ramadhan Saidi amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kusema kuwa wana mikakakati thabiti ili kuweza kuondoa changamoto hiyo

Sauti ya mwenyekiti

Aidha mwenyekiti wa bodi ya  maji wilayani uvinza bw sayaredi nyamtongo amesema  kuwa wana mpango wa kujenga tanki la maji ambalo litakua limerahisisha upatikanaji wa maji katika kijiji hicho

Sauti ya mwenyekiti

Hata hivyo Maji katika kijiji cha ruchugi imekua changamoto kubwa hali inayopelekea kununua dumu la maji la lita 20 kwa sh 500 hasa katika msimu huu wa kiangazi