Uvinza Fm

Corona yaathiri Wafanyabiashara wa samaki na dagaa

05/07/2021, 5:55 pm

Na,Glory Paschal

Baadhi  ya Wavuvi  na Wafanyabiashara wa Samaki na Dagaa Mkoani Kigoma Wamesema Kufungwa kwa Mipaka ya Nchi Jirani  Kutokana na Maambukizi ya Ugonjwa wa Corona Kumeathiri Biashara zao

wafanyabiashara wa dagaa na samaki

Wavuvi  Pamoja na Wafanyabiashara ambao Wamesema hali ya biashara imekuwa Ngumu Kutokana na Idadi Kubwa Ya Wafanyabiashara Kutoka Nje ya Nchi Waliokuwa Wakifika Katika Mialo ya Dagaa Na Samaki Mkoani Kigoma Kushindwa Kuingia Kutokana na Mipaka yao Kufungwa.

Wamesema iwapo Serikali  itasaidia  Kuzishawishi Nchi Hizo  Kulegeza Masharti kwa Wafanyabiashara Wanaoingia na Kutoka Katika Nchi Hizo itasaidia kupunguza changamoto hizo.

Sauti za wafanyabiashara wa samaki na dagaa

Afisa  Biashara Mkoa wa Kigoma Deogratius Sangu licha Ya Kukiri Kuwepo Kwa Changamoto za Kibiashara Baada Ya Kufungwa kwa Mipaka Lakini Ameshauri  Wavuvi na Wafanyabiashara Kuheshimu Taratibu Zilizowekwa Katika Kukabiliana na Ugonjwa Huo.

Sauti ya Afisa biashara