Uvinza Fm

Mradi wa maji kakonko wafikia asilimia 65

01/06/2021, 4:26 pm

Na,Rosemary Bundala

Serikali imesema hadi kufikia disemba 2020 tayari miradi kumi na tano ilikuwa inatekelezwa katika wilaya ya kakonko ambapo miradi kumi na nne imekamilika na inatoa huduma ya maji kwa wananchi na mradi mmoja uliobaki ni mradi wa kakonko ambao utekelezwaji  wake umefikia asilimia  65 na unatarajia kuhudumia mji wa kakonko pamoja na kijiji  cha kasuga

Naibu waziri wa maji Mhandisi Maryprisca Mahundi

Hayo yamejiri  leo bungeni  jijini  Dodoma wakati Naibu waziri wa maji mhandisi  Maryprisca  Mahundi alipokuwa  akijibu  swali la mbunge wa buyungu mh Aloyce john kamamba lililohoj ni kwanini miradi ya maji ya kakonko haijakamilika kwa muda mrefu na lini mji huo na vitongoji  vyake utapata majisafi na salama na ya kutosha

Sauti ya naibu waziri wa maji

Naibu maji  01Aidha mh mahundi amesema kuwa mradi wa maji wa kakonko unatekelezwa na Ruwasa kwa kutumia wataalamu wake wa ndani kwa ajili ya kuukamilisha mradi huo ambapo mchakato huo unafanyika kwa awamu

Sauti ya naibu waziri wa maji

Katika hatua nyingine mh Mahundi amesema katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 serikali pia imepanga kujenga miradi mipya katika vijiji vya chilambo na kokinonko ,ukarabati na utanuzi wa mradi wa muhange kwenda muhangejuu na shule ya sekondari ndalichako pamoja na kuchimba visima virefu katika vijiji viwili vya chilambo na nyakiobe

Sauti ya naibu waziri wa maji

Bunge limeendelea leo jijini Dodoma ambapo waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa afrika mashariki Liberata Mulamula anatarajiwa kuwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha  2021/2022 na wabunge watapata nafasi ya kujadili  kile ambacho kitakuwa kimewasilishwa.