Uvinza Fm

Shilingi 7.3bilioni kutengeneza mtandao wa barabara

23/04/2021, 4:15 pm

UVINZA

Na,Editha Edward

Wananchi katika wilaya ya UVINZA mkoani Kigoma wameiomba serikali kupitia TARURA kuongeza kasi katika ujenzi wa barabara ya Uvinza mjini ili Kuruhusu shughuli za kiuchumi za wananchi kufanyika kwa urahisi

Barabara ikiwa kwenye matengenezo

Wakizungumza na Radio Uvinza Baadhi yao wamesema Pamoja na jitihada zilizopo za TARURA kujenga miundombinu ya barabara Bado kuna maeneo yasiyopitika kutokana na ukosefu wa madaraja katika Baadhi ya Mito jambo linaloathiri shughuli zao zikiwemo za Biashara Kufayika

Sauti za Wananchi Uvinza

Mratibu wa TARURA mkoa wa Kigoma Mhandisi Godwin Mpinzile amesema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 kiasi cha shilingi bilioni 7.3 kimeidhinishwa kwa ajili ya ujenzi wa mtandao wa barabara na madaraja kwa mkoa wa Kigoma huku milioni 400 kwa mwaka 2021 zikiwa zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa madaraja wilaya ya Kigoma ambapo hadi sasa madaraja 15 yamekamilika na ifikapo Juni mwaka huu madaraja 20 yanatarajiwa kuwa yamekamilika

Sauti ya Mratibu wa TARURA Kigoma