Uvinza Fm

Kilio cha Walemavu chatatuliwa

16/04/2021, 3:35 pm

UVINZA

Na, Editha Edward

Baada ya Redio uvinza fm kuripoti taarifa ya watu wenye ulemavu kupatiwa mikopo  ya asilimia 10 inayotolewa na kila halmashauri  kwa takribani miezi mitano iliyopita  ili kujikwamua kiuchumi halmashauri ya wilaya ya uvinza mkoa wa kigoma imetoa mkopo kwa makundi maalumu wanawake,vijana na watu wenye ulemavu zaidi ya milioni Themanini

Baadhi ya watu wenye ulemavu wakikabidhiwa hundi na mkuu wa mkoa kigoma

Akizungumza  katika hafla ya utoaji mikopo hiyo iliyofanyika jana katika ukumbi wa biashara uliopo wilayani hapa mkuu wa mkoa wa Kigoma kamishina wa polisi THOBIAS ADENGENYE ambaye ndo alikuwa mgeni rasmi amesema mikopo hiyo iliyotolewa kwa makundi hayo itawasaidia na kuwabadilisha maisha yao  endapo pesa hizo watazifanyia shughuli za kimaendeleo

Sauti ya Mkuu wa Mkoa Kigoma

Naye mkuu wa wilaya ya Uvinza Bi.MWANAMVUA HOZA MRINDOKO amesema vijana na watu wenye ulemavu  wamekuwa hawajitokezi kwa wingi katika fursa hiyo ya  kuchukua mikopo hivyo amewataka kujitokeza ili waweze kunufaika

Sauti ya Mkuu wa Wilaya Ya Uvinza

Kwa upande wao wanufaika wa mikopo hiyo ambao miongoni mwao  ni watu wenye ulemavu wamesema wanaishukuru serikali kwa kuwathamini licha ya kuwachukua muda mrefu wa kupata mikopo hiyo  tangu walipoiomba

Sauti za Walemavu

Aidha halmashauri ya Wilaya uvinza imefanikiwa kutoa mikopo kwa makundi maalumu ikiwa ni  asilimia mia moja tangu sheria ya fedha ilipofanyiwa marekebisho.