Sibuka FM

Wanaoishi maisha duni hatarini kupata ugonjwa wa kifua kikuu

21 March 2023, 12:47 pm

Imeelezwa  kuwa  Jamii  inayoishi  katika  Makazi  Duni   ipo hatarini  kuugua  Ugonjwa   wa  Kifua  kikuu  kutokana  na  hali  zao za  Maisha   na  Mfumo  wa  Maisha  wanayoishi..

Hayo  yameelezwa  na   Mratibu  wa Mapambano  dhidi  ya  Kifua  Kikuu  kutoka Muungano  wa  Wadau wa Kupambana  na  Kifua  Kikuu  Tanzania   Nelson  Terekela   Wakati  wa  Mafunzo  ya  Kuwajengea  Uwezo  waandishi  wa  Habari  wa  Mkoa  wa  Simiyu  kuhusu  Ugonjwa  wa  Kifua  kikuu  na  Matibabu yake.

Sauti ya Nelson Terekela

      

Nelson  amesema  kuwa mara  nyingi  watu  wenye  makazi  Duni miundo mbinu  ya  Mzunguko  wa  Hewa na  Mwanga  wa  kuingia  na  Kutoka  unakuwa  haupo  hali  ambayo inaweza kupelekea  kuambukizana  kama  mmoja wenu  ana  Ugonjwa   wa  Kifua  kikuu.

Sauti ya Nelson Terekela

     

Emmanuel  John  ni  Mratibu  wa  Kifua  kikuu  na  Ukoma   Mkoa  wa  Simiyu  amesema  kuwa  Mkakati  wa  Mkoa  ni  kuwatafuta  na  Kuwaibua  wagonjwa ambao  hawajabainika   na  kuwaweka  kwenye Matibu  ili  wasiendelee  kuambukiza  watu  wengine  kwani  Ugonjwa  wa  Kifua  kikuu  huambukizwa  kwa  njia  ya  Hewa.

Sauti ya Emmanuel John- Mratibu wa TB Simiyu

    

Aidha  kwa  Upande  wake  Mratibu  wa  Kitaifa  wa Masuala ya  Uraghbishi, Mawasiliano  na Uhamasishaji  kutoka  Mpango  wa  Taifa  wa Kifua  kikuu  na Ukoma  Ndugu  Julias  Mtemahanji  amesema  kuwa  lengo ni  kuelekea  katika  Maadhimisho  ya  siku  ya  kifua  kikuu  ambapo  Mgeni  Rasmi  anatarajiwa  kuwa  Waziri  Mkuu   wa  Jamhuri  ya  Muungano wa  Tanzania   Mh, Kasimu Majaliwa.

Sauti ya Julias Mtemahanji

   

Baadhi  ya  waandishi  walioshiriki  Mafunzo  hayo Samweli Mwanga na Annastazia Paul wamesema  kuwa  watatumia  kalamu  na  Taaluma  zao  katika  kuielimisha  Jamii  kuhusu  Ugonjwa  wa  TB  na  namna  ya kukabiliana  na  Ugonjwa  huo.

Sauti za Baadhi ya Waandishi walioshiriki