Sibuka FM

Wilaya ya Maswa kuandikisha Watoto wa Darasa la Awali 13,000 kwa Mwaka wa Masomo 2023

15 December 2022, 4:47 pm

Imeelezwa  kuwa  Wilaya  ya  Maswa   Mkoa  wa  Simiyu  hadi  kufikia   mwezi  Novemba , 2022  Imefanikiwa Kuandikisha  Watoto  wa  Darasa  la  Awali   Elfu  Saba (7000)  Sawa  na  Asilimia  Hamsini  na  Mbili (52%)  ya  Makisio  yote  ya  Watoto   Elfu  kumi  na  tatu (13000)  Wanaotarajiwa   kuandikishwa  Darasa  la  Awali  Mwaka  2023..

Hayo  yameelezwa  na  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Maswa  Mh,  Aswege  Kaminyoge   wakati  akitoa  Taarifa  juu  Uandikishaji  wa  Watoto  Wilayani  hapo  Mkuu  wa  Mkoa  wa  Simiyu  Dkt   Yahaya  Nawanda  alipofanyaziara  ya  Kutembelea  na  kukagua  Ujenzi  wa  Vyumba  vya  Madarasa  kwa  ajili  ya  Wanafunzi   wataojiunga  mwaka  2023.

Katika  watoto  wa  Darasa  la  kwanza  Mh   Kaminyoge  amesema  kuwa   hadi   Novemba  30, 2022 walikuwa  wameandikisha  Watoto  Zaidi  ya  Elfu  kumi na moja  (11000)   Sawa  na  Asilimia  68%    Kati  ya  Makadirio  ya  kuandikisha  zaidi  ya watoto  Elfu Kumi  na  Sita (16000).

Aidha   Mh  Kaminyoge  Amesema  kuwa  katika  Ujenzi  wa  Vyumba  wa  Madarasa  Jumla  ya  shule  29  kati  ya  33   zimeshakamilisha  ujenzi  wa   vyumba  vya  madarasa  huku   vyumba  4  vikiwa  katika  hali ya  Ukamilishaji wa  Sakafu  na  uwekaji  wa  madirisha  ya  Alminium.

Kwa upande  wake  Mkuu  wa  Mkoa  wa  Simiyu  Dkt   Yahaya  Nawanda  amempongeza  Mkuu  wa  Wilaya  na  Timu  yake  kwa  zoezi  la  Uandikishaji  wa  Watoto  na  Kumtaka  hadi  kufikia  Tarehe 20  mwezi  huu awe  amekamilisha  ili  mwezi  Januari  Wanatoto waanze Masomo  bila  wasiwasi.

Mh  Dkt  Nawanda  amefanya  ziara  ya  Ukaguzi  wa  vyumba  vya  Madarasa  katika  Shule  ya  Sekondari  Nyalikungu, Shule  ya  sekondari   Kinamwigulu, Shule  ya  Sekondari  Buchambi  Pamoja  na  Shule  ya  Sekondari  Zanzui  kisha  kumalizia  Mkutano  wa  Hadhara  wa  Kupokea  Kero  za  Wananchi  katika  Uwanja  wa  Madeko  Mjini  Maswa.

 

Hapa  chini  ni  picha  za  Matukio  ya  Ziara  ya  Mh  RC  Nawanda