Sibuka FM

UZAZI WA MPANGO UNASAIDIA KUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI.

29 November 2022, 6:24 pm

Imeelezwa  kuwa   matumizi  ya  Uzazi  wa Mpango yanasaidia kupunguza  kwa   asilimia  kubwa  vifo  vitokanavyo  na  Uzazi  kwa  akina  mama..

Hayo  yameelezwa  na  Dr  Boniface  Mabonesho  Mtaalamu  wa  Masuala  ya   Afya  ya  Uzazi  kutoka  Zahati  ya  Mwagala  iliyopo Wilayani  Maswa  Mkoani  Simiyu  wakati  akizungumza  na  Radio  Sibuka  Fm..

Dr  Mabonesho  amesema  kuwa   mama  anapokuwa  na  utaratibu  wa  kuzaa  kwa  Mpango  inasaidia  mwanamke  kuimarisha  Afya   yake  kabla  ya  kubeba  Ujauzito  mwingine..

Amesema  kuwa  Jamii  imekuwa  na  Mtazamo  hasi  kuhusu  Uzazi  wa  Mpango  “ Jamii  imekuwa  na  Mtazamo  hasi  kuhusu  Uzazi  wa  Mpango na  kuamini  kuwa  njia  hizo  zimekuwa  zikisababisha  Ugumba  kwa  Wanawake’’

‘’Ni  vizuri  Jamii  ikaelewa  kuwa  njia  za  Uzazi  wa  Mpango  hazisababishi  Ugumba  pengine  wanatumia  bila  kufuata  utaratibu na ushauri   kutoka  kwa  madaktari  wanapotaka  kutumia  njia  hizo’’

Joyce  Masanja  ni  mama  wa  watoto  wawili  kutoka  kijiji  cha  Mwanhonoli  kilichopo  wilaya  ya  Maswa  amesema   kuwa njia   za  Uzazi  zimemsaidia  kuzaa  watoto  kwa  kuwapishanisha   umri  na  kuweza  kuwahudumia  vizuri..

‘’Watoto  wangu   Anitha  na   Emmanueli  niliwapishanisha  kwa  muda  wa  miaka minne(Anita nilimzaa mwaka 2016 mwezi wa 3 na Emmanuel nilimzaa 2020  Mwezi  wa  7)  hali  iliyonipa kuwa  na  muda  mwili  kujijenga  na  kunipa  nafasi  ya  kufanya  shughuli  zingine  za  kiuchumi”