Sibuka FM

Mila Kandamizi Zatajwa kuchangia Vifo vitokanavyo na Uzazi Wilayani Maswa..

29 October 2022, 6:23 pm

Imeelezwa  kuwa  Mila  kandamizi  kwa   baadhi  ya  Jamii  ikiwemo  kabila  la  Wasukuma  zinachangia  vifo vitokanavyo  na  Uzazi  kwa  Wanaume Kushindwa  kushiriki  na Wenza  wao kikamilifu  katika  Huduma  ya  Afya  ya  Uzazi.

Hayo  yameelezwa  na   Mkurugenzi  wa  Shirika  lisilo  la  kiserikali  la  Kawiye  Social  Development  Foundation- KASODEFO  Marius  Isavika  wakati  akitoa  Elimu juu  ya  Mila  Potofu  zinavyochangia   Vifo  kwa   akina  Mama  wajawazito   kupitia  Radio  Sibuka  fm.

Isavika  amesema  kuwa   Jamii  ya  Wasukuma   hasa  kwa  wanaume  wamekuwa   hawashiriki  masuala  ya  Afya   ya  Uzazi  ikiwemo  kwenda  kiliniki  na  mwenza  wake  nikujidhalilisha  na  kujishushia  hadhi kwa  mwanaume..

‘’Kwa sisi  wasukuma  kwenda  na  mke  wako  kiliniki  nikujidhalilisha  kwasababu  Jamii  itakuona  umeshikwa  na  Mwanamke au  kuonekana  mwanaume  Bwege   Jambo  ambalo   siyo  sahihi  kwa  Ulimwengu  wa  Sasa’’

‘’Ni  vizuri  Jamii  yetu  ikaelewa  kuwa  masuala  ya   Afya  ya  Uzazi  na  Uzazi  wa  Mpango  ni  ya  wote   Baba  na  Mama   kushirikiana  pamoja   kwa  kwenda  kwenye  vituo  vya  kutolea  Huduma  za  Afya  na kukaa  chini   na  kuamua muzae watoto  wangapi  na  siyo jukumu  la  mama  pekee  yake’’

‘’Ninatoa   wito  kwa   Wananchi  hasa  Wanaume  Wilayani  Maswa  na Mkoa  wa  Simiyu  kwa  Ujumla  kwasababu  Sibuka  fm  inasikika  sehemu  Tofauti  kubadilika na  kuondoa  Mila  Potofu  zinazochangia  kwa  sehemu  kubwa  vifo  vya   akina  Mama  Wajawazito’’

Elias  John  na   Masanja  Mabula  ni  Baadhi  ya  Wanaume  waliozungumza  na  Sibuka  Fm  Radio  wamekiri  kutokushirikiana  na  Wenza  wao  katika   Masuala  ya  Afya  ya  Uzazi  kwakuwa   Masuala  ya  Uzazi  hayawahusu  hivyo  kuanzia  sasa  baada  ya  kupata  Elimu  hiyo  watashiriki  kikamilifu  ili  kupunguza  vifo  vitokanavyo  na  Uzazi..

‘’ Haya  Masuala  ya  kusindikiza  Wenza  wetu  kiliniki  tulikuwa  tunaona  kuwa  hayatuhusu  sisi  Wanaume ,  lakini  kumbe  yana  Umuhimu  sana  katika  kusaidia  kupunguza  Vifo vitokanavyo  na  Uzazi  kuanzia  sasa  hatutapuuza  baada  ya  Elimu  hii’’