Sibuka FM

WAFUGAJI WILAYANI MASWA WAASWA KUFUGA MIFUGO KISASA ZAIDI ILI KULETA TIJA

2 September 2022, 5:44 pm

Mwenyekiti  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya   Maswa   Mh   Simoni   Maige   Amewataka   Wafugaji  kufuga   Mifugo   kwa  Tija  ili  ilete   Manufaa  na  kuwakwamua   Kiuchumi..

Mh  Maige   ameyasema  hayo   wakati  wa  Uzinduzi  wa  Josho  la  kuogeshea   Mifugo  lililojengwa  katika  Kijiji  cha  Dodoma  kilichopo  kata  ya  Mwamashimba  Wilayani  Maswa  na  kuwataka  wananchi  kuondokana  na  Utamaduni  wa  kufuga  Ng’ombe   Wengi  lakini  hawana  Manufaa  kwao..

Amesema  kuwa  Wafugaji  wengi  wamekuwa  wakiishi  maisha  magumu  huku  wakiwa  na  Mifugo  Mingi  hali  ambayo  mifugo  hiyo  imegeuka  kuwa  Adhabu   badala  ya  kuwasaidia   kuwakwamua  kiuchumi  na  Kipato..

Awali  akitoa  Taarifa   ya  Utekelezaji  wa   Ujenzi  wa  Josho  hilo   Afisa  Mifugo  na  Uvuvi  wa  Halmashauri  ya  Wilaya  ya  Maswa  Dkt   James  Kawamala  amesema  kuwa  Josho  limegharimu  kiasi  cha  Shilingi Milioni 19  ambapo  nguvu  ya Wananchi  ni  Shilingi  Milioni 1.7  Huku  Fedha  nyingine  zikitoka  Serikali  kuu..

Aidha   Dkt  Kawamala  amesema  kuwa   Josho  hilo  litaogesha  Wanyama  Zaidi  ya  Elfu Tano Wakimo  Ng’ombe, Mbuzi  na  Kondoo   Hivyo  kuweza  kuokoa  Vifo  vya  Mifugo  hiyo  vitokanavyo  na  Magonjwa  ya  Kupe  na  Wadudu  wengine  ambao  wanachangia    kwa  Zaidi  ya  Asilimia  80.

Nao   baadhi  ya  Wafugaji  wakawa  na  haya  ya  Kusema   huku  wakiishukuru  Serikali  kwa  kuwaletea  huduma  hiyo  kwani  hapo  Awali  walikuwa  wanapata  Shida  kuogesha   Mifugo  yao   huku  Mwenyekiti   wa  Kijiji  hicho  akiahidi  kuitunza  na  kuilinda  Miundo   hiyo  kwa  nguvu  zote.

 

Haapa  chini  picha  za  matukio  ya  Uzinduzi  wa  Josho  la  kuogeshea mifugo.