Sibuka FM

BUSEGA YAPIGA HATUA KUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI KUTOKA VIFO 145 MWAKA 2017 HADI 41 KWAKA 2021.

25 May 2022, 6:52 pm

Idara ya Afya katika Wilaya ya Busega, mkoani Simiyu, kwa kipindi cha miaka mitano imefanikiwa kupunguza vifo vya mama na mtoto kutoka 145 mwaka 2017 hadi 41 mwaka 2021.

Hayo yamesema  na  Mratibu  wa  Huduma  ya Afya ya  Mama Baba  na  Mtoto  Wilayani Busega  Joseph  Katitweze  na Muuguzi mkuu  Irene  Sembo    Wakati wakitoa  taarifa  Katika  Maadhimisho ya  siku  ya  Wauguzi  Duniani.

Wamesema kuwa , wanajivunia kupunguza vifo vya mama na mtoto kutoka 145 mwaka 2017 hadi 41 mwaka 2021, Huku akitaja  malengo  ni  kufikia vifo sifuri  ifikapo 2025.

Insert  01.  Joseph  Katitweze  na  Irene  Sembo   Wakieleza  namna  walivyopunguza  vifo vya  Uzazi

Aidha  Mratibu  huyo  wa  Huduma  ya  Afya ya  Mama Baba  na Mtoto  ameeleza  changamoto zinazowakabiri  katika kutimiza majukumu yao na  kuhakikisha hapatokei  kifo  kinachotokana  na  Uzazi  kwani  Uzazi  siyo  Ugonjwa..

   Insert  02. Joseph  Katitweze   akielezea   changamoto zinazowakabili

Naye  Mkuu wa Wilaya ya Busega Gabriel  Zakaria na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Wilaya hiyo,  Bi  Veronica Sayore, wameahidi kutatua baadhi ya changamoto zilizondani  ya  Uwezo  wao  ili kutengeneza mazingira rafiki kwa watumishi hao

Insert  03.  Mkuu  wa  Wilaya ya   Busega  na  Mkurugenzi  mtendaji  wakielezea  namna  watakavyotatua  changamoto za  wauguzi..

Siku ya wauguzi husherehekewa Mei  12 kila Mwaka, ikiwa kumbukumbu ya kuzaliwa muasisi  kada hiyo  Florence Nightngale, ambaye ni mwana takwimu na mwanzilishi wa uuguzi wa kisasa.

 

.

Insert  01.  Joseph  Katitweze  na  Irene  Sembo   Wakieleza  namna  walivyopunguza  vifo vya  Uzazi

.

Insert  02. Joseph  Katitweze   akielezea   changamoto zinazowakabili

.

Insert  03.  Mkuu  wa  Wilaya ya   Busega  na  Mkurugenzi  mtendaji  wakielezea  namna  watakavyotatua  changamoto za  wauguzi..