Sibuka FM

RC KAFULILA AAGIZA KUONDOLEWA KWA MENEJA WA WAKALA WA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA VIJIJINI – RUWASA WILAYANI MASWA KWA KUSHINDWA KUSIMAMIA MIRADI YA MAJI…

19 May 2022, 5:24 pm

Mkuu  wa  Mkoa  wa  Simiyu  Mh  David  Zacharia  Kafulila  ameagiza  kuondolewa  Meneja  wa  Wakala wa  Maji   na  Usafi  wa  Mazingira  vijijini   wilayani   Maswa   Lucas  Madaha  kwa  Kushindwa   kusimamia  miradi  ya   Maji  ambayo  imekuwa  ikitolewa  na  Serikali..

Mh  kafulila  ametoa   maagizo  hayo  wakati  wa  Ziara  yake  ya  kukagua   Miradi  ya  Maji  na  Barabara  wilayani   hapa  na  kusema  kuwa  meneja  huyo   inabidi  abadilishwe  kutoka  na   Uwezo  wake   mdogo  wa  kusimamia  miradi  ya   Maji  ambayo  imekuwa  ikiletwa  na  serikali ya  Awamu  ya   Sita   kwa  ajili  ya  kusaidia   wananchi  wake.

Insert  01.   RC   Kafulila  Maswa.

Amesema  kuwa  miradi  mingi  imekuwa  ikichukuliwa   na  wakandarasi  wakubwa  na  kuwapa  mafundi  wadogo  ambao  hawana  ujuzi  wa  kutosha  kisha  wao  kuendelea  na  kazi  zingine  hivyo  kupelekea  miradi  kujengwa  chini  ya  kiwango  na  kutaka  mikataba  yote  iliyosainiwa  makao  makuu  iletwe  hapa  mkoa  simiyu  ili  ipitiwe  upya  na  iwe  rahisi kufuatilia ..

Insert   02.   RC  Kafulila  Maswa…

Baadhi  ya  wananchi  wa  Kizungu  wilayani  Maswa   wakapata  nafasi  ya  kumweleza    adha  wanayopata  kutokana  na  ukosefu  wa  Maji  licha  ya  Serikali  kutoa  Fedha  nyingi  kwa  ajili  ya  kuwaondolea  Adha  wananchi  ya  kutembelea  Umbali  mrefu…

Insert  03.  Wananchi wa  Kizungu-Maswa

Meneja   wa   RUWASA   wilaya  ya  Maswa  Lucas  Madaha   amesema  kuwa  Miradi  mingi  ilichelewa  kuanza  utekelezaji   kutokana  na kusubiri   msamaha  wa    VAT  kwa   vifaa  vya  Ujenzi  wa  Miradi  hiyo..

Insert  04.  Lucas   Madaha-Meneja  RUWASA