Sibuka FM

Vijana  Jitokezeni  katika  Vituo vya  Huduma  Rafiki  ya Afya  ya  Uzazi. 

28 March 2022, 10:19 am

Vijana  wameaswa  kujitokeza  katika  Vituo  rafk  vya  kutolea  huduma  za  Afya  ili  kupata  Elimu  zaidi kuhusu  masuala mbalimbali  ya  Afya  na   Afya  ya  Uzazi.

Hayo  yamesemwa  na  Dr Godfrey Christopher kutoka Kituo  cha  Afya  Muungano  kilichopo Wilayani  Bariadi  Mkoani  Simiyu  Wakati  akitoa  Elimu  ya  afya  ya uzazi  kwa  vijana  na  Umuhimu  wake   kupitia  Sibuka  fm  na  kusema  vituo  hivyo  ni  muhimu  kwani  ni  sehemu  sahihi  ya  kupata  Taarifa  sahihi..

Sauti ya Dr Godfrey Christopher

         

Akitoa  fafanuzi  kuhusu  huduma  Rafiki  za  Afya  ya Uzazi kwa  vijana  Dr Christopher amesema  kuwa   huduma  hizo  hutolewa  kwa  Usalama  na  Ufanisi  wa  hali  ya  juu  hivyo  vijana  wajitokeze  kwa   wingi  kupata  Elimu  kuhusu  Afya  ya  Uzazi  na  Uzazi   wa  Mpango.

Sauti ya Dr Godfrey Christopher

         

Michael Luvinga  ni Mratibu  wa  Huduma  Rafiki  ya  Afya ya Uazi kwa  vijana   amesema  kumekuwa  na  mafanikio  makubwa  toka  kuanzishwe  kwa   vituo  hivyo   vya  Huduma  rafk  ya  Afya  ya  Uzazi  kwa    Vijana  Ukilinganisha  na  hapo  Awali .

Sauti ya Michael Luvinga