Sibuka FM

Mtoto afariki baada ya kujeruhiwa na Fisi-Maswa.

9 September 2021, 1:20 pm

Mtoto mwenye umri wa miaka 5 anayejulikana  kwa  jina  la  Masule. S. Cosmas mkazi wa kijiji cha  zawa   kata  ya  mwanghonori wilayani  Maswa  Mkoani Simiyu   amefariki baada ya kujeruhiwa na  fisi  sehemu mbalimbali za mwili wake.

Tukio hilo limetokea  Siku ya Jumatano tarehe  8.9.2021 majira ya saa 15:00 alasiri.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa polisi Mkoa wa Simiyu Richard  Abwao  amesema kuwa tukio hilo limetokea wakati  mtoto huyo akiwa na wenzake ambao ni Naomi  Amosi na Scholastika  Wahumija,

Wakiwa wanachunga ng`ombe na mbuzi kwenye maeneo ambayo yapo mbali na makazi yao, ndipo fisi huyo alitokea na kuanza kuwakimbiza na kufanikiwa kumkamata Mtoto  huyo  Masule   Cosmas na kuanza kumshambulia baadhi ya viungo vya mwili ambavyo ni shavu la kulia na kumtoa ngozi ya kichwa pamoja na macho yote mawili kitendo kilichopelekea kifo chake.

Jitihada za kumtafuta fisi huyo zilifanywa na wananchi na kufanikiwa kumpata na kumuua.

 Mwili   wa Marehemu  umefanyiwa uchunguzi na daktari na baadaye kukabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya mazishi.

Jeshi la polisi Mkoa wa Simiyu linatoa  wito kwa Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kwa watoto wao  dhidi ya wanyama wakali  kwenye maeneo yao hasa vijijini.