Sibuka FM

Maji ya Ziwa Victoria kuleta suruhisho la changamoto ya maji mji wa malampaka-Simiyu.

22 July 2021, 10:47 am

Mkurugenzi  Mtendaji  wa  mamlaka  ya  maji  na  Usafi wa  mazingira  Maswa- MAUWASA   Mhandisi   Nandi  Mathias  amesema  kuwa   kuanza  kutekelezwa  kwa  mradi  wa  maji  kutoka  ziwa  Victoria  utaondoa  changamoto  ya  Upatikanaji  wa  Maji  katika  katika  Mji  wa  Malampaka  uliopo wilayani  Maswa   Mkoani  Simiyu.

Mhandisi  Nandi  amesema  kuwa  mji wa  malampaka  unawakazi  zaidi  ya  Elfu  kumi  na  tano   ikiwa  mahitaji  ya  maji  kwa  siku ni  Lita  za  Ujazo  milioni moja  hali  inayopelekea  kuwa  na  Upungufu  ikilinganishwa  na  Uzalishaji wa  maji  kwa  siku..

Sauti ya Mhandisi  Nandi  Mathias -Mauwasa

        

Pichani Mkurugenzi wa Mauwasa-Mhandisi Nandi Mathias.

Amesema  kuwa  changamoto  zilizojitokeza wakati  wa  Mkutano wa  hadhara  wa  mkuu wa  mkoa  kwa  baadhi  ya  wananchi  kusema  visima  havitoi  maji  siyo  kweli   kwani   visima  hivyo kwa  sasa  vinafanya  kazi  na walivifufua    baada  ya  kukabidhiwa  kutoka   kwa  Wakala  wa  Usambazaji  maji  na  Usafi  wa  Mazingira  vijijini –RUWASA.

Sauti ya Mhandisi  Nandi  Mathias -Mauwasa

          

Yona  Gabriel  Swale  na  Angela  Masunga  ni  wasimamizi  katika  pampu  za  kusukuma   maji  katika  mji wa  malampka wamesema  kuwa  changamoto  ya  maji  ipo  ikilinganishwa  na  wingi  wa  Watu licha  ya  wao   kusukuma  maji  kwa  wakati..

Wahudumu wa pampu za maji malampaka

            

Aidha   baadhi  ya  wananchi  wamezungumza  Radio  Sibuka  na  kusema  kuwa  hali  ya  upatikanaji  wa  maji  kwa  sasa  katika  mji  huo  ni  nzuri  ikilinganishwa  na  hapo  awali  maji  yalikuwa  ya  shida  upatikanaji  wake.

Baadhi ya wananchi- malampaka

         

Hapa chini picha mbalimbali..