Sengerema FM

Serikali yaagiza kufukiwa kwa mashimo yanayotokana na uchimbaji madini

8 April 2021, 3:28 pm

Naibu waziri ofisi ya makamu wa rais mh.Hamad Hassan Chande akijibu swali Bungeni

Serikali imesema mashimo makubwa yote yaliyotokana na uchimbaji wa madini katika Mikoa ya Mara, Geita na Shinyanga yanapaswa kufukiwa ili kurejeshwa katika hali yake ya awali.

Hayo yamebainishwa na leo bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Hamad Hassan Chande wakati akijibu swali la Mbunge wa Bunda Mhe. Boniface Getere.

Katika swali hilo alitaka kufahamu mikakati ya Serikali ya kufukia mashimo makubwa yaliyosababishwa na ulimaji wa barabara na uchimbaji wa madini hasa katika mikoa hiyo.

Akiendelea kujibu swali hilo Mhe. Chande alisema Sheria ya Mazingira Na. 20 ya Mwaka 2004 inaelekeza maeneo yaliyoharibiwa kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini kurejeshwa katika hali yake awali ikiwemo kufukia mashimo, kupanda miti na kudhibiti taka.