Radio Jamii Kilosa

Watoto wanaishi katika mazingira magumu walia na Serikali -Kilosa

13 March 2021, 4:30 am

Watoto wanaishi katika mazingira magumu walioko Kata ya magomeni Wilayani Kilosa Mkoani Morogoro amba wanafahamika kwa jina la Magomeni Children Development Machide wamomba serikali na wadau mbalimba kuwatazama katika jicho la huruma ili kuwasaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazo wakabili katika kupata huduma Kama vile maradhi,chakula na elimu.

Wameyasema hayo machi 6 2021 walipo tembelewa na Uongozi wa Radio Jamii Kilosa wakati walipokuwa wakusoma lisala yao kwa mgeni rasmi wakati wa kusherekea kumbukizi za kuanzishwa Radio Jamii Kilosa ikiwa inatimiza miaka 15 toka kuanzishwa kwake Machi 6 2006.

Wamesema kuwa watoto wamesajiliwa kwajina la Magomeni Children Development MACHIDE lakini hakuna kituk ambacho kinawakusanya pamoja ili waweze kupata huduma kwani kwa Sasa waishi majumvani na wazazi walezi Babu au Bibi ambao hawana wezo wa kuwapatia mahitaji hivyo waneiyomba Serikali na wadau kuwanengea kituo ili iwe rahi kupata huduma kutoka Serikalini na wadau kwa ujumla.

Akizungumza katka sherehe hizo katibu wa Machide Christopha Chusi mesrma kuwa mbaka sasa machide ina watoto 25 wenye umri kuanzia miaka 1.5 hadi 16 Kati yao wasichana ,,,,wavurana,,, wanaosoma shule ya Sekondari,,,msingi ,,, na ambao Hawa somi ,,,

Naye meneja wa Radio Jamii Kilosa Gladys Mapeka ambaye aliambatana na wafanyakazi wake amesema kuwa kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwa ni pamoja na kutoa zawadi kwa watoto hao Kama vile sabuni,mafuta ya kupaka, nguo ,juice,mayai,na biskuti lengo ni kuwapa faraja watoto hao wenye uhitaji. Kufanya usafi katika hospitali ya Wilaya kilosa ikiwa ni pamoja na kuchangia damu ikiwa kuunga mkono juhudi za serikali katika sekta ya afya inayotaka kuwa na bank ya damu kwa ajili ya kusaidia watu wenye uhitaji.

Kwauoandewake Dr ,,,,,,,,,,amesema kuwa anaishukuru Radio Jamii Kilosa kwa kuazimisha kumbukumbu ya radi kwa kufanya usafi katika jengo hilo kwani usafi katika mazingira ya hospitali ni muhimu sana hasa katika kipindi hiki kigumu ambacho tunaishi kwa tahadhari kubwa kuhusu magonjwa ya mlipuko.

Dr amesema kuwa walio jitokeza kuchangia damu walikuwa tisa saba Kati yao wamechangia jumla ya chupa saba wawili Kati yao walikosa sifa kulingana na u hache wa damu ambapo amesema kuwa amefurahishwa na tukio hilo kwani Kutoa damu kwa ajili ya watu wengine ni Jambo la kujitoa kwa moyo hivyo ametoa wito kwa wananchi kujenga maeya ya kuchangia damu au kunda clabu za wachangia damu kwa hospitali ya Wilaya bado inauhitaji mkubwa wa damu .

Naye Diwani wa kata ya Magomeni ambaye pia ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika Sherehe hizo ameahidi kuwapatia kupatia kiwanja Machide ili kituo kijengwa na kuwaomba Viongozi kuendelea kufuatilia kwa kina kubaini watotowengine ambao ni yatima ili waweze kulekewa katika kituo hicho.