Pangani FM

Tree of Hope wabaini haya Pangani

27 March 2023, 12:23 pm

Shirika lisilo la Kiserikali TREE OF HOPE lenye makao yake makuu

jijini Tanga limekutana na wadau wa elimu katika vijiji vya Ubangaa,

Stahabu, Kipumbwi na Mkalamo katika mdahalo uliolenga kujadili

changamoto za elimu wilayani Pangani.

Akizungumza na Pangani FM baada ya mdahalo huo Afisa Programu kutoka shirika hilo Bw. GoodluckMalilo amesema katika siku hizo mbili

ya midahalo wamefanikiwa kubaini mafanikio ya kuandikishwa shule

kwa Watoto wenye ulemavu, pamoja na wazazi kuchangia walimu wa

kujitolea.

Sauti ya Goodluck Malilo.
Goodluck Malilo kutoka Shirika la Tree of Hope.

Bwana Malilo  amesema kuwa  kutokana na mdahalo huo wamebaini kuna

changamoto ya kutokuwa na walimu mahsusi wa watoto wenye mahitaji

maalumu katika shule zilizopo katika vijiji hivyo.

Awali wakizungumza wakati wa mawasilisho washiriki katika mdahalo

huo, wa vijiji vilivyotembelewa wameeleze jinsi mradi wa uwajibikaji,

na elimu jumuishi umewawezesha wao kujitambua na kuona wanao

wajibu wa kushughulikia changamoto za elimu zilizopo vijijini kwao .

Shirika la Tree of Hope inaendesha mradi unaolenga uwajibikaji,

uboreshaji wa elimu na elimu jumuishi kwa vijiji vinne, huku katika

Mdahalo huo wa siku mbili Jumatano na Alhamisi ukiwashirikisha

wadau mbalimbali ikiwemo viongozi wa vijiji, walimu, waratibu elimu

kata, maafisa maendeleo kata, viongozi wa dini na wananchi.