Pangani FM

Mkuu wa wilaya atoa agizo hili katika Sheria Pangani.

2 February 2023, 9:01 pm

Mkuu wa wilaya ya Pangani Bi.Zainab Abdallah Issa akizungumza katika Kilele cha wiki ya Mahakama. Picha na Ofisi ya DC Pangani

Na Saa Zumo kushirikiana na Erick Mallya

Kauli mbiu ya wiki ya Sheria mwaka 2023 ni ‘Umuhimu wa Utatuzi wa Migogoro kwa Njia ya Usuluhishi Katika Kukuza Uchumi Endelevu: Wajibu wa Mahakama na Wadau.’

Mkuu wa wilaya ya Pangani Bi. Zainab Abdallah amemuagiza mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo Bw. Issaya Mbenje kutenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa mahakama ya kisasa.

Agizo hilo amelitoa  katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria wilayani Pangani yaliyofanyika katika vwanja vya mahakama ya wilaya pamoja na kuahidi kutoa kipaumbele kwa masuala ya Mahakama ili kurahisisha upatikanaji wa haki kwa wananchi Pangani.

“Bila kuishika hii tasisi na mhimili huu muhimu hatuwezi kwenda kwa sababu kama wanadamu lazima kutatokea ukiukwaji wa sheria na migongano sasa hiki chombo ndio kinasaidia kufanya utatuzi na usuluhishi”

Amesema Bi.Zainab Abdallah Issa