Nuru FM

Dhamana Kizungumkuti Iringa

3 March 2023, 4:18 pm

Picha ikimuonesha mtuhumiwa.Picha kwa msaada wa mtandao.

Wameomba elimu hiyo mara baada ya kupata usumbufu ambao wamekuwa wakipitia wakati mgumu wakifuatilia dhamana.

Na Joyce Buganda.

Wakazi wa Manispaa ya Iringa  wameiomba Serikali kuendelea kutoa elimu kuhusu  suala la  dhamana ili kuwapunguzia adha pindi wanapohitaji huduma hiyo.

Wakizungumza na kituo hiki baadhi ya wananchi wamesema baadhi yao hawatambui vyema mchakato wa kupata dhamana kwa mtuhumiwa jambo linalosababisha usumbufu kwao hivyo kutolewa kwa elimu kutawasaidia kuokoa gharama.

Wananchi wa manispaa ya Iringa wakielezea swala hilo.

Kuhusu suala hilo wakili  Cleofas Mwailuka amsema mtu mwenye kuanzia miaka 18 ana haki ya kumdhamini mtuhumiwa pia  kuna elimu ya dhamana  ambayo huwa inatolewa kila mwezi februali kila mwaka katika wiki ya sheria pamoja na kufanya majukumu mengine kuelimisha uma.

Wakili  Cleofas Mwailuka akitoa elimu kuhusu dhamana.

Aidha amtaja makosa kama ya mauaji  uharifu kwa kutumia silaha na kutaka kuipundua serikali hayana dhamana na kuionya jamii kutojihusisha na makosa ya aina yoyote.

Wakili  Cleofas Mwailuka akieleza kuhusu watuhumiwa wasiostahili dhamana.

Kwa mujibu  wa sheria  ya mwenendo wa makosa ya jinai kifungu cha 148 kifungu kidogo cha 5 kimeainisha makosa mengine ambayo mtuhumiwa akipewa dhamana ni hatari kwa usalama wake  makosa hayo ni pamoja na ulawiti, utakatishaji fedha, kusafirisha dawa za kulevya na ugaidi.