Nuru FM

Kinana kumrithi Mangula

31 March 2022, 4:55 pm

Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM iliyokaa leo Machi 31, 2022 mkoani Dodoma imepitisha kwa kauli moja jina la aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama hicho Abdulrahman Kinana kuwa Makamu mwenyekiti wa chama hicho Tanzania Bara, baada ya aliyekuwa akishika nafasi hiyo, Philip Mangula kung’atuka.

Hayo yamesemwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Shaka Hamdu Shaka alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya mkutano wa NEC.

Jina la kinana litapitishwa na wajumbe wa Mkutano mkuu maalum unaotarajiwa kufanyika April Mosi, katika ukumbi wa Jakaya Kikwete uliopo Mkoani Dodoma.