Mpanda FM

Serikali Kutatua Mgogoro wa Kagera Group Dhidi ya Wanakijiji Dirifu

6 April 2023, 8:46 am

MPANDA

Serikali imehaidi kutatua mgogoro uliopo kati ya bodi ya kagera group na wanakijiji wa dirifu kata ya magamba ,manispaa ya mpanda mkoani katavi.

Hayo yamesemwa na katibu tawala wa manispaa ya Mpanda Kenneth Pesambili akimwakilisha mkuu wa wilaya ya Mpanda ambapo amesema kuwa serikali ipo kwa ajili ya wananchi na wapo tayari kutatua changamoto hiyo.

Kwa upande wake Afisa utawala wa wilaya ya mpanda Gilbert Bagaya amewaomba wananchi wawe wavumilivu ili serikali iendelee kutatua changamoto hiyo.