Mpanda FM

Watembea kwa Miguu Walia na Waendesha Vyombo vya Moto

16 September 2022, 4:07 am

MPANDA

Baadhi ya watembea kwa miguu katika manispaa ya  mpanda mkoani katavi wamewalalamikia madereva wa vyombo vya moto kutozingatia sheria na alama za usalama barabarani pindi wanapoendesha.

Wakizungumza na mpanda redio fm wananchi hao wameeleza kuwa wanakutana na changamoto ya  kunyimwa uhuru wa kutumia barabara kwa kuhofia kusababishiwa ajali na madereva  kwa kutozingatia alama za usalama barabarani.

.

Kwa upande wake askari wa usalama barabarani kutoka ofisi ya RTO John Shindika amesema kuwa idadi kubwa ya madereva ambao hawazingatii alama za usalama barabarani ni wale ambao hawajasoma udereva na kusema kuwa jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani hakitasita kumchukulia hatua za kisheria  kwa yeyote atakae vunja sheria za usalama barabarani.

.

Hivi Karibuni kumeripotiwa Ajali nyingi ambazo zimetokana na baadhi ya madereva kutozingatia sheria na alama za usalama barabarani .