Mpanda FM

Wananchi Watakiwa Kuwa Wavumilivu Maboresho ya Barabara

8 September 2022, 6:49 pm

IVUNGWE- MPANDA

Siku chache tangu barabara ya ivungwe kuanza kurekebishwa kwa ahadi ya mbunge Sebastiani Kapufi wananchi wametakiwa kuwa wavumilivu wakisubiri kumalizika kwa mradi huo kutokana na changamoto ya kuharibika kwa mtambo wa kutengeneza barabara hiyo.

Akizungumza kwa  njia ya simu Mwenyekiti wa kijiji cha Kasokola Carlos  Joackim  Mwalufa  amesema utekelezaji wa barabara hiyo ulishaanza katika baadhi ya maeneo ya  Ivungwe .

.

Awali  Wananchi  wakizungumza na Mpanda radio fm walisema  kuwa kwa kipindi kirefu wamekuwa   wakichelewa kupata huduma ya afya kwa haraka kutokana na ubovu wa barabara   kufika zahanati kupata huduma ya afya na kuomba serikali kuwasadia kuboresha barabara.

.

Kuboresha kwa barabara kutoka ivungwe -kasokola umeanza  kutekelezwa baada ya ziara ya mbunge wa jimbo la Mpanda mjini Sebastian Kapufi Ivungwe kusikiliza kero za wananchi ambapo wamekuwa wakitumia barabara iliyoharibika kufuata huduma ya afya takribani kilomita kumi katika kijiji cha kasokola.