Mpanda FM

HAKI ZA WATOTO ZIZINGATIWE

8 June 2022, 4:14 pm

Jamii imetakiwa kutambua kuwa Ajira kwa watoto zina athiri malengo na afya zao kiujumla .

Wakizungumza na mpanda fm wakazi wa halmashauri ya Manspaa Mpanda wamesema kuwa ziko familia ambazo zinawafanyisha kazi watoto hali inayodhorotesha afya za watoto hao.

Sambamba na hilo wamewataka wazazi na walezi kuzingatia kuwapatia watoto haki yao ya msingi ambayo ni elimu.

Kwamujibu wa inspekta  Kelvin fuime kutoka dawati la jinsia mkoa wa katavi mtoto ni Yule mwenye umri kuanzi miaka0 hadi 18 hivyo hatakiwi kujishughulishan na shughuli yoyote ya kujipatia kipato hivyo ni  wajibu wa mzazi kuhakikisha mtoto anapata mahitaji yake yote muhim ikiwa ni pamoja na kumpatia elimu.