Mazingira FM

TANAPA: Upigaji faini mifugo inayoingia hifadhini bado sio ‘mwarobaini’ kwa wafugaji

17 May 2023, 6:23 pm

Upigaji wa faini kwa mifugo inayoingia katika maeneo ya hifadhi bado sio mwarobaini wa kukomesha vitendo vya wafugaji kuingiza mifugo katika maeneo ya hifadhi hususani katika kipindi cha kiangazi.

Kamishna Msaidizi wa TANAPA Kanda ya Magharibi Albert Mziray

Hayo yamesemwa na Kamishna Msaidizi wa Tanapa Kanda ya Magharibi, Albert Mziray wakati akizungumza na Radio Mazingira Fm ofisini kwake jana tarehe 16 May 2023 kufuatia malalamiko ya baadhi ya wafugaji kukamatiwa mifugo yao inayoingia hifadhi na kupigwa mnada.

Mziray amesema utaratibu uliokuwepo ni kutoza faini ya shilingi laki moja (100,000) kwa kila mfugo lakini utaratibu huo bado haujafanikiwa kukomesha vitendo hivyo kwani adhabu inaonekana ni ndogo kwa wafugaji na kufanya vitendo hivyo kuendelea hususani katika kipindi cha kiangazi na wakati mwingine inaipa hifadhi kazi kubwa ya kuitunza mifugo baada ya wafugaji kukimbia.

Amesema kwa sasa yapo maelekezo ya serikali kwamba mifugo hiyo inapokamatwa ndani ya hifadhi itaifishwe na kupelekwa mahakamani kisha inapigwa mnada.

Albert Mziray

Mziray amesema zipo changamoto za mifugo kuingia kwenye maeneo ya hifadhi na kusababisha athari mbalimbali ikiwa ni pamoja na ushindani wa kupata malisho kwa wanyamapori na magonjwa kutokana na mwingiliano wa wanyama wa kufugwa na wanyama pori.

Albert Mziray