Mazingira FM

Ahukumiwa Jela Maisha kwa kosa la kumbaka mtoto wa Miaka 7

12 May 2023, 8:03 am

Mahakani wilayani Bunda imemuhukumu kifungo Cha Maisha Jela Melkiadi Mgaya,umri 22years, mkulima,mkazi wa mtaa wa Balili Bunda kwa kosa la kumbaka mtoto wa Miaka 7 kwa nyakati tofauti.

Kesi hiyo namba 238/2022 ya Kubaka, imetolewa hukumu May 10, 2023

Inaelezwa hakamani hapo na mwendesha Mashtaka wa polisi Tryphone Makosa Jacob kwamba mtuhumiwa amekuwa akimbaka mtoto wa kike umri 07 years, jina limehifadhiwa toka mwaka 2020 hadi tarehe 22/12/2022 alikutwa na Babu wa mhanga akiwa amempakata huku akimbaka.

Kesi ilifikishwa mahakamani 29/12/2022 mbele ya Mheshimiwa Mulokozi Paschal Kamuntu hakimu mkazi Mfawidhi Mwandamizi wa mahakama ya wilaya na kusomewa mashitaka ambapo mshitakiwa alikana na ushahidi ulitolewa.

Tarehe 10/05/2023 amehukumiwa kwenda jela maisha baada ya mahakani kujilidhisha pasi na shaka kwamba mtuhumiwa alitenda kosa hilo angalia akijua ni kinyume na Sheria Kifungu 130 (1),(2) (e) na 131 (3) Kanuni ya adhabu sura 16 marejeo 2022

Awali Mwendesha mashitaka wa Polisi mkaguzi msaidizi wa polisi Tryphone Makosa Jacob amesema katika kesi hiyo Mashahidi 05 waliletwa upande wa mashtaka hivyo aliiomba mahakama kumpa adhabu kali kwa Mujibu wa kifungu cha sheria aliyoshtakiwa nayo Ili liwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo.

Naye mshtakiwa katika utetezi wake aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwani ni mkosaji wa mara ya kwanza na kwamba yeye ni mlemavu na hana wazazi