Mazingira FM

Bei ya pamba msimu wa 2022/2023 hadharani

11 May 2023, 6:40 pm

Wakulima wa zao la pamba watauza pamba yao kwa bei ya ukomo isiyopungua 1060 kwa msimu wa mwaka 2022 na 2023.

Hayo yamesema wa makaguzi wa zao la pamba wilayani Bunda Hemedi Kabea alipozungumza na Mazingira Fm iliyofika ofisini kwake kwalengo la kujua iwapo msimu wa pamba umefunguliwa ama la!.

Kabea amesema msimu wa zao la pamba tayari umefunguliwa kitaifa tangu tarehe 2 mwezi may mkoani Kigoma katika wilaya ya Kasuru ambapo bei ya kianzio ni 1060 kwa kilo lakini kampuni itakayopewa kipaumbele ni ile itakayokuwa na bei nzuri.

HEMEDI KABEA

Aidha amesema mkulima hatokatwa fedha ya pembejeo alizokopeshwa na bodi ya pamba badala yake atapokea fedha yake kama ilivyo .

HEMED KABEA

Kabea ameongeza kuwa kwa wilaya ya Bunda msimu bado haujafunguliwa kwa kuwa wanasubili miongozo itakayotumika katika msimu huu lakini maandalizi yote tayari yamefanyika ikiwemo ukaguzi wa mizani, uandaaji wa maghala ya kuhifadhia pamba miongoni mwa mengine.