Mazingira FM

Kesi 104 za ukeketaji wilayani Tarime hazikufika mwisho kwa kukosa ushahidi

27 April 2023, 7:19 pm

Timu ya waandishi wa habari wa kupinga Ukeketaji

imeelezwa kuwa ukeketaji unaovuka mipaka bado ni changamoto hasa katika jamii zinazoishi mipakani kati ya nchi na nchi.

hayo yamebainishwa katika ufunguzi wa warsha ya mafunzo kwa Waandishi wa habari za kupinga masuala ya ukeketaji unaovuka mipaka inayofanyika wilayani tarime mkoani Mara.

akizungumza katika warsha hiyo afisa utawi wa jamii kutoka wilayani tarime Antony Nyange amesema suala la ukeketaji unaovuka mipaka ni tatizo kubwa katika maeneo yanayopakana kati ya taifa moja na lingine kwa kuwa jamii kutoka pande zote katika mipaka ni za aina moja.

“tumekumbana na changamoto kubwa kupambana katika suala hili unakuta kiongozi anaishi upande mmoja wa nchi lakini anawaongoza wa hata wale kutoka upande wa pili wa nchi wajamii ile ile”.

“unakuta upande wa mama ni Kenya ila upande wa baba ni Tanzania hivyo ugumu unakuja pale ambapo unakutana na mtoto mpakani unadhani anavuka kwenda kukeketwa ia ukimkamata anakwambia anakwenda kwa mjomba au shangazi hivyo inakuawa ngumu kuendelea kuwashikilia” amesema Antony .

kwa upande wake Valeriani Mgani ambaye meneja miradi wa kituo cha AT-FGM MASANGA kilichopo tarime mkoani Mara amesema katika mataifa matano katika ukanda wa afrika mashariki walipitisha makubaliano 9 mnamo 17 /4/2019 ambayo yanatekelezwa katika mataifa yote matano.

Valeriani ameongeza kuwa mataifa hayo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Ethiopia pamoja na Somalia ambapo amesema kwa mwaka 2021 hadi 2022 kesi 104 za ukeketaji zilizoripotiwa wilayani Tarime na kufikishwa mahakamani ila hakuna kesi hata moja iliyofika mwisho na kutolewa hukumu kutokana na kukosa ushahidi.

Pia kwa miaka mitatu iliyopita yaani 2019 hadi 2022 zaidi watoto 287 wamekimbilia Tanzania wakitokea kenya kukwepa ukeketaji.

Naye Michael Marwa ambaye ni kutoka shirika la C-SEMA amesema wameandaa warsha hii ikiwa lengo ni kuwajengea uwezo waandishi wa habari kupaza sauti katika vita hii ya ukeketaji unaovuka mipaka .