Dodoma FM

Wafanyabiashara wa mbogamboga walalamika bishara ngumu

19 April 2023, 5:42 pm

Wauzaji wa mbogamboga katika soko la Majengo.Picha na Thadei Tesha.

Hii inafuati msimu wa mvua za mazika ambazo zimekoma hivi karibuni Mkoani hapa hivyo watu wengi wenye maeneo wameotesha mbogamboga mbalimbali na kuzipa kisogo mbogamboga za sokoni.

Na Thadei Tesha.

Wafanyabiashara wa mbogamboga wamelalamikia kudorola kwa soko la mboga hizo kutokana na wanunuzi wengi kuotesha mboga nyumbani.

Licha ya kushamiri kwa mbogamboga sokoni bado hali ya upatikanaji wa wateja sio ya kuridhisha je nini sababu inayopelekea changamoto hiyo baadhi ya wauzaji wa bidhaa hiyo wanaeleza zaidi

Sauti za wafanyabishara wa mbogamboga

Aidha kwa upande wao baadhi ya wananchi jijini Dodoma wanasema kuwa kufuatia msimu wa mvua kumepelekea watu wengi kupanda mbogamboga majumbani hivyo kupelekea mwitikio wa kununua mboga hizo kuwa mdogo.

Wauzaji wa mbogamboga katika soko la Majengo.Picha na Thadei Tesha.
Sauti za wananchi

Katika baadhi ya masoko jijini Dodoma upatikanaji wa bidhaa za mbogamboga ikiwemo tembele mchicha na chinese imeonekana kushamiri zaidi kwa hivi sasa.