Dodoma FM

Wananchi watumie kumbukizi ya siku zao za kuzaliwa kupanda miti

3 March 2023, 2:05 pm

Wadau wa mazingira kutoka shule za Sekondari. Picha na Seleman Kodima.

Hatua hii inatoa tafsiri ya moja kwa moja na kuhitaji uhamasishaji wa pamoja wakufikia azma  serikali ya  Lengo la  kupanda miti 5,075,000, katika kipindi cha miaka minne.

Na Selemani Kodima

Wito umetolewa kwa wananchi jijini Dodoma kutumia kumbukizi ya siku zao za kuzaliwa kwa kupanda miti ili kuhakikisha tunafanikiwa kutumiza malengo ya mendeleo Endelevu ya utunzaji wa mazingira

Wito huo umetolewa na Mwalimu Malick Masoud mdau wa mazingira na mratibu wa shirika routs and shoots mkoa wa Dodoma ambaye ameamua kutumia siku yake ya  kumbukiza ya kuzaliwa kama sehemu ya kutoa wito kwa jamii kuhusu umuhimu kwa kupanda miti.

Wadau wa mazingira kutoka shule za Sekondari. Picha na Seleman Kodima.

Mwl Masoud anasema ameamua kufanya hivyo ili kuonesha umuhimu wa upandaji wa miti kwa jamii na utekelezaji wa vitendo azma ya serikali ya kukijanisha dodoma  na sera ya mazingira ya mwaka 2021 ya kuhakikisha kila kaya inapanda miti mitano.

Sauti ya Mwalimu Malick Masoud mdau wa mazingira na mratibu wa shirika routs and shoots mkoa wa Dodoma

Katika zoezi hilo  la upandaji miti ambalo  ilikuwa ni sehemu ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa ya Mwl huyo lilihudhuriwa na baadhi ya wadau wa mazingira ,Walimu wa mabingwa wa mazingira kutoka baadhi ya shule jijini Dodoma na hapa baadhi yao wanaelezea lengo la watu kuona umuhimu wa upandaji wamiti.

Sauti za wadau wa mazingira.