Dodoma FM

Changamoto ya umeme yakwamisha maendeleo kata ya Loje Chamwino

2 February 2023, 2:01 pm

Nguzo ya umeme ikiwa imeanguka. Picha na mtaa kwa mtaa Blog

Kuanguka kwa nguzo za umeme katika baadhi ya maeneo yenye huduma ya umeme katika kata ya Loje imetajwa kusababisha kukosekana kwa kuhuduma hiyo .

Na Victor Chigwada

Wananchi wa kijiji cha Ingunguli Kata ya Loje Wilaya ya Chamwino wameiomba Serikali kuwasambazia huduma ya umeme katika vitongoji vyao ili kuondokana na adha ya matumizi ya huduma hiyo

Hamisi Msangi ni mwenyekiti wa kijiji Ingunguli   amesema kuwa pamoja na baadhi ya vitongoji kukosa huduma hiyo lakini changamoto nyingine ni kuanguka kwa nguzo za umeme  maeneo yenye huduma hiyo.

Hamis Msangi

Naye Diwani wa Kata ya Loje Bw.John  Njohoka amekiri upatikanaji wa huduma ya umeme kwa kijiji cha Igunguli bado ni hafifu licha jitihada zinazo endelea  kufanywa ikiwemo kuhakikisha huduma hiyo inawafikia wananchi

John Njohoka.