Dodoma FM

Wananchi watakiwa kushiriki awamu ya tatu ya chanjo

1 September 2022, 2:19 pm

Na; Benard Filbert.

Licha ya awamu ya pili ya utoaji wa chanjo ya Polio kufanikiwa kwa asilimia 100 ,Jamii imeombwa kutoa ushirikiano katika zoezi hilo ambalo limeanza leo kwa awamu ya tatu.

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi Rosemary Senyamule wakati akizungumza na wajumbe wa kamati ya chanjo ya polio ikiwa siku ya kwanza ya zoezi hilo.

Ameipongeza kamati hiyo  kwa kazi nzuri waliyofanya awamu ya pili huku akiwataka kufanya hivyo katika awamu ya 3.

.

Hivi karibuni Bi Lotaris Gadau afisa mradi mpango wa taifa wa chanjo ya Polio akizungumza na Dodoma Tv Amesema kuwa Tanzania imejitahidi kwa kiasi kikubwa kuzuia magonjwa yanayozuilika kwa chanjo kwani hadi hivi sasa hakuna kisa chochote ambacho kimeripotiwa kutokana na ugonjwa wa polio.

.

Baadhi ya wananchi wamezungumza na taswira ya habari wamesema mpango huo ni mzuri kwani utawalinda watoto kupata maambukizi ya polio ambayo madhara makubwa .

.

Chanjo ya polio inatolewa kwa watoto chini ya miaka 5 lengo kuwapa kinga dhidi ya virusi vya polio huku ikielezwa kuwa mtu mmoja akibainika kuwa na kirusi cha polio kuna uwezekano wa watu zaidi ya mia mbili kupata kirusi hicho.