Chai FM

kilio uhaba wa maji Rungwe kupata tiba mwezi oktoba

9 September 2022, 10:15 am

RUNGWE-MBEYA

NA:WANDE BUSHU

Wananchi wa Kitongoji cha Kawetele chini Wilaya ya  Rungwe Mkoani Mbeya wameiomba serikali kuwatatulia changamoto ya huduma ya maji iliyo dumu kwa muda mrefu licha la kulipia bili ya maji kila mwezi

Wakizungumza na Chai Fm wamesema  kuwa hali ya kukosekana kwa maji katika kitongoji hicho kunaweza kuleta athari kama vile mlipuko wa magonjwa yanatokana na uchafu wa mazingira kutokana na kukosekana kwa Maji.

Tusubhilege  Mwasoni na William  Banda ambao ni wakazi wa Mtaa huo wamewaomba Viongozi  husika kuwasaidia  kuepukana na adha ya maji wanayokumbana nayo kwani imewalazimu kutembea umbali mrefu kufata huduma hiyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kitongoji Alphonce  Mwabhulondo amesema amezungumza  na viongozi wa mamlaka bila kupewa ushirikiano wowote hivyo anaendelea kuiomba idara husika kutatua changamoto hiyo.

Kwa upande Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya maji Tukuyu  mjini  Bw  Peter Amon amesema kufikia tarehe 30 mwezi wa kumi  mwaka huu wananchi watapata maji kwa utoshelevu  kwani maboresho ya miundombinu ya maji inaendelea kufanyiwa marekebisho.